Habari zilizopatikana jana zinasema marehemu Adonis alikuwa akisumbuliwa na ini kwa muda mrefu, ambako alikuwa akipatiwa matibabu katika hospitali hiyo hadi mauti yalipomkuta afajiri ya jana.
Mbali ya kung'ara na Yanga katikati ya miaka ya 1980, Adonis alikuwa akiichezea timu ya Veterani ya Yanga, ambako mara ya mwisho kuidakia ilikuwa mwaka jana jijini Dar es Salaam dhidi ya watani wao Simba Veterani.
Adonis ambaye alikuwa mwajiriwa wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), pia alikuwa ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Soka Wilaya ya Arusha (ADFA) na mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), akiwakilisha klabu za Mkoa wa Arusha.
Marehemu ameacha mke na watoto kadhaa. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi.
No comments:
Post a Comment