Saturday, January 05, 2008

Kikosi kurejea leo

Wawakilishi wa Tanzania Bara katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, Yanga wanatarajiwa kurejea nchini leo kutoka Afrika ya Kusini ambako iliweka kambi ya mazoezi kwa muda wa wiki 3.

Kwa mujibu wa Katibu Mwenezi wa klabu hiyo Francis Lucas ambaye aliambatana na timu hiyo, amesema Yanga inatarajia kutua nchini leo na kesho itaelekea Zanzibar kwa ajili ya kushiriki katika michuano ya Kombe la Mapinduzi.

Ikiwa huko Afrika ya Kusini, Yanga ilicheza mechi nne za 'mazoezi' dhidi ya timu za madaraja ya chini. Timu nyingi za madaraja ya juu za huko, zipo katika mapumziko ya mwisho wa mwaka hivyo Yanga ilishindwa kupata mechi yeyote ya maana ya kujipima nguvu.


No comments: