Yanga katika kundi A
Mabingwa watetezi wa kombe la Tusker - Yanga imepangwa katika kundi A pamoja na timu za URA ya Uganda na Mtibwa Sugar ya Turiani (TZ).Mabingwa wa zamani wa michuano hiyo, Simba wapo katika kundi B pamoja na timu za Prisons ya Mbeya (TZ) na Tusker ya Kenya.
Ratiba kamili ya michuano hiyo ambayo bingwa wake atajinyakulia kitita cha shilingi milioni 40 ni kama ifuatavyo:
Desemba 15: URA vs Mtibwa Sugar (Kundi A)
Desemba 16: Prisons vs Tusker (Kundi B)
Desemba 17: Yanga vs URA (Kundi A)
Desemba 18: Simba vs Prisons (Kundi B)
Desemba 20: Yanga vs Mtibwa Sugar (Kundi A)
Desemba 21: Simba vs Tusker (Kundi B)
Desemba 23: Nusu Fainali (1A vs 2B)
Desemba 24: Nusu Fainali (1B vs 2A)
Desemba 26: Kutafuta mshindi wa Tatu na Nne
Desemba 27: Fainali
Michezo hiyo inatarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa Taifa wa zamani.
1 comment:
ratiba mbaya wangetupanga kundi moja na simba tuwafundishe adabu.
Post a Comment