Saturday, October 03, 2009

Vita vya Kagera
Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Vodacom Yanga leo wanajitupa katika Uwanja wa Kaitaba huko Kagera kupambana na Kagera Sugar ya huko katika mchezo wa ligi hiyo.

Yanga inabidi iingie kwa umakini katika mchezo huo, kwani katika misimu miwili iliyopita ilitoka kapa katika uwanja huo.

Michezo mingine inayopigwa leo ni:
Simba vs Moro United
Mtibwa Sugar vs Prisons
Toto Africa vs Majimaji

19 comments:

Anonymous said...

cm lete raha kaka mdau buruda hapa

Anonymous said...

bado hamna matokeo ndugu?

Anonymous said...

Dar Simba wanaongoza kwa goli 1

Bukoba, mambo bado...Kagera Sugar wamekosa penati.

CM said...

Yanga wamepata bao katika dakika ya 26 kupitia kwa Mrisho Ngassa.

Kagera 0 Yanga 1

CM said...

Dakika ya 55 bado tunaongoza 1-0.

Katika Uwanja wa Uhuru Simba 1 Moro United 1

CM said...

Yanga imepata bao la pili kupitia kwa Jerson Tegete.

Kagera 0 Yanga 2

Anonymous said...

Asante cm mwendo mdondo kaka !!!!!!!!! MYAMA LAZIMA ALIWE LEO

Anonymous said...

? Mpira bado haujaisha

Anonymous said...

mnyama kapata bao la 2

CM said...

Mpira umekwisha Dar:
Simba 2 Moro Utd 1

sp said...

pointi 18 safi kwa mnyama.

Anonymous said...

Hakuna wa kumzuia MNYAMA mwaka huu, ote lazim walie tu!!!

Anonymous said...

Tusiangalie mnyama, sisi tuendelee kushinda tu...mnyama lazima atapoteza points huko mbeleni sisi tuendelee kushinda ndiyo dawa. Tuwe kama Man U, jamaa wenyewe wanachoangalia ni ushindi tu mpaka mwisho wa Ligi, huu ni mpira wa miguu, ligi bado sana.

Judy,

Denmark

CM said...

Mpira umekwisha huko Kaitaba kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Kagera Sugar.

Kwa ushindi huo Yanga sasa imefikisha pointi 11.

Jioni njema

Anonymous said...

Tusiangalie mnyama, sisi tuendelee kushinda tu...mnyama lazima atapoteza points huko mbeleni sisi tuendelee kushinda ndiyo dawa. Tuwe kama Man U, jamaa wenyewe wanachoangalia ni ushindi tu mpaka mwisho wa Ligi, huu ni mpira wa miguu, ligi bado sana.

Judy,

Denmark

Kwi! Kwi! Kwi! Dua la kuku halimpati mwewe!!! eti yeboyebo kama Man u!! Subirini kichapo tu mtakapokutana na Mnyama

Mwalala

NY

Anonymous said...

wee judy mjinga sana ,man yuu ni wakubebwa tuu,unamaana nanyi yeboyebo mnabebwa sio? check leo match yao na sunderland utapata jibu, mnyela mkubwa weeee

Anonymous said...

Mdau hapo juu naona umechoka kubeba maboxi unamalizia hasira kwa Judy....nenda kapumzike bwana. Majuu kuzuri kama umesoma...

Tina said...

hahaha mnanifurahisha sana wana simba midomo juuu kazi mnayo.hata mseme sana ligi bado sna tu angalia msije kulia!yanga oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

Anonymous said...

cm na wanayanga wenzangu hivi ule mpango wa ngasa kwenda tena ktk majaribio westham umeishia wapi?wakati ule tuliambiwa ataludi tena kwa majaribio mengine ,lini ataludi tena westham?