Saturday, November 28, 2009

Ambani, Hamisi warejeshwa

Klabu ya Yanga imewarejesha wachezaji wake wawili Boniface Ambani na Hamisi Yusuf ambao ilitangaza kuwaacha hivi karibuni................................................................................................................
Kurejeshwa kwa Ambani na Yusuf kunafuatia wachezaji hao kukosa timu ya kuchezea na hivyo kulindwa na kanuni ya usajili ya TFF inayolazimisha mchezaji ambaye mkataba wake utasitishwa wakati wa dirisha dogo la usajili kurejeshwa katika timu yake ya zamani endapo atakosa timu nyingine ya kuchezea.............................................................................................................
Wachezaji wengine walioachwa katika dirisha dogo la usajili Mike Barasa (amemaliza mkataba) na Joseph Shikokoti (amepata timu huko Kenya). Vicent Barnabas ameuzwa kwa mkopo kwa timu ya African Lyon.

2 comments:

Anonymous said...

haya sasa wathibitishe kama kweli kiwango kipo au hakipo.

Anonymous said...

Hapo ndo inathibitisha namana gani viongozi wasivyokuwa makini, halafu tunategemea viongozi hawa hawa wawe na mikakati madhubuti ya kuhakikisha timu inafanya vizuri. sijui