Wednesday, January 30, 2008

Yanga yatoa 7 Taifa Stars

Chuji - amerejeshwa Taifa Stars

Timu ya soka ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imetangazwa hapo jana huku Yanga ikitoa wachezaji 7 kuunda kikosi hicho.

Akitangaza kikosi hicho hapo jana, Kocha Mkuu wa Taifa Stars Marcio Maximo amemrejesha kiungo Athumani Iddi "Chuji" katika kikosi hicho. Kurejeshwa kwa Chuji katika kikosi hicho kulitegemewa na wengi kufuatia kiwango kizuri cha uchezaji alicho nacho hivi sasa.

Wachezaji wengine kutoka Yanga wanaounda kikosi hicho ni Amir Maftah, Nadir Haroub "Cannavaro", Castory Mumbala, Abdi Kassim, Jerry Tegete na Vincent Barnabas.

Taifa Stars inajiandaa na mchezo wa kujipima nguvu dhidi ya Malawi utakaopigwa tarehe 6 mwezi ujao katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Kila la heri vijana wetu.

No comments: