Saturday, February 23, 2008

Yanga kuwania uongozi leo

YANGA, ambayo tangu kuanza kwa duru la pili la Ligi Kuu haijapoteza pointi, leo itakuwa ikiwania kurejea kileleni mwa msimamo itakapokutana na ndugu zao wa Toto Africans kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Lakini, vinara Prisons wanaweza kurejea kileleni kesho iwapo wataishinda timu inayosuasua ya Simba.

Yanga, ambayo ilipokonywa ubingwa wa Bara kwenye Ligi ya Mpito mapema mwaka jana, inashika nafasi ya pili baada ya kukusanya pointi 33, ikiwa imezidiwa na Prisons kwa pointi moja na ushindi ukipatikana leo utaifanya ifikishe pointi 36.

10 comments:

Anonymous said...

Leo tunaongoza lakini kwa muda maana kesho prisons anampa kipigo mnyama.

Anonymous said...

Vipi matokeo?
mdau -Berks, UK

Anonymous said...

Tumeshinda 2-1

Anonymous said...

asante hii ni raha tupu.na wiki ijaayo mtu atakula 5-0.

Anonymous said...

poa nashukuru kwa matokeo lakini naomba majina wa wafungaji wetu

Anonymous said...

Mkuu bado tunaongoza au???Prisons leo imekuaje??

Anonymous said...

Prisons wamefungwa 3-1 leo, kwa hiyo tunaendelea kuongoza huku tukiwa na mechi moja mkononi.

Anonymous said...

Saafi saana.,

Hapa kilichobaki ni kuendelea kukusanya point 3 kila mechi hadi kwenye ubingwa, maana simba tayari wamerahisisha kazi.

Anonymous said...

Huyu jamaa wa UK poa sana maana anafuatilia mambo ya Bongo mpaka raha. Keep it up wote wa majuu.

Baba Kelvin wa Temboni.

said...

You have a most interesting blog.

Stay on groovin’ safari,
Tor