Saturday, October 17, 2009

Yangaic vs Azam FC


Kocha mpya wa Yanga Kosta Papic leo anapata mtihani wake wa kwanza kwa kupambana na Azam FC katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom kwenye Uwanja wa Uhuru.
Yanga inakumbana na moja ya timu ngumu katika ligi hiyo kwani ina wachezaji kadhaa ambao wanaweza kusumbua katika mchezo wa leo.

Mshambuliaji John Boko wa Azam ndiye anayeongoza orodha ya wafungaji katika ligi hiyo. Timu hiyo pia ina beki wa kutegemewa wa Taifa Stars Salum Sued pamoja na viungo wazoefu kama Shaban Kisiga. Azam inanolewa na kocha msaidizi wa zamani wa Taifa Stars, Itamar Amorin.
Hata hivyo kwa vyovyote itakavyokuwa, wachezaji wa Yanga hawatataka kumwangusha kocha wao mpya kutoka Serbia ili aweze kuwa na mwanzo mzuri katika kukisuka kikosi hicho.
Yanga na Azam zote zina pointi 14.
Katika michezo mingine ya ligi hiyo, Majimaji itaikaribisha Manyema FC ya Dar, Prisons itakuwa nyumbani dhidi ya Toto Africa.
Matokeo ya mechi za leo:
Yanga vs Azam 1-1
Prisons vs Toto Africa 1-1
Majimaji vs Manyema 0-0