Saturday, September 11, 2010

Ligi Kuu ya Vodacom

AFC yaipania Yanga
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania inaendelea leo kwa mechi mbili ambapo Yanga itakuwa ugenini dhidi ya AFC ya Arusha katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid huku Azam na Simba zikiumana katika Uwanja wa Mkwakwani huko Tanga.

Kwa muda wa wiki sasa, AFC imekuwa ikijigamba kuifunga Yanga katika mchezo wa leo ili irudishe imani ya wapenzi wake baada ya kuanza vibaya ligi hiyo. Beki wa zamanai wa Yanga ambaye amejiunga na AFC, Hamis Yusuf 'Waziri wa Ulinzi' ameitahadharisha Yanga kutotarajia mchezo mwepesi leo.

Yanga bado inakabiliwa na wachezaji majeruhi kama Shamte Ally na Kiggi Makasy. Hata hivyo mshambuliaji Kenneth Asamoah amepona hivyo anatarajiwa kuteremka dimbani leo kuwavaa AFC.

16 comments:

Anonymous said...

mambo magumu au?

Anonymous said...

mnyama kisha mlamba azam 2-1

Anonymous said...

nani anajali?

Anonymous said...

kwani hii blog ya azam au simba?

Anonymous said...

acheni hasira mahanithi nyie

Anonymous said...

huyu mzenji katoka wapi?

Anonymous said...

kikawaida baadhi ya watu huona watu wote kama wao sasa msishangae nae maana yeye ndivyo alivyo

Anonymous said...

cm kaka mambo yakoje hapo? tuko mbali huku

Anonymous said...

AFC 2 YANGA 1[Tegeta]

Anonymous said...

kwani na wewe ni cm?????? au mnyama unataka nikereheke?

Anonymous said...

ha ha ha ha ha ha ha walete walete

Anonymous said...

Katika mchezo mwingine wa Ligi kuu ya Vodacom uliofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha jioni ya leo yanga imefanikiwa kuifunga timu ya AFC ya Arusha magoli mawili kwa bila. Magoli hayo yamefungwa na wachezaji Ernest Boake na Iddi Mbaga na kuifanya Yanga kujipatia pointi tatu muhimu kama mahasimu wao Simba

Anonymous said...

habari ndio hiyo watasema watatukana lakini ushindi huo safi kabisa

Anonymous said...

AFC 0 Yanga 2
Azam 1 Simba 2

Anonymous said...

Wajameni matokeo ni
AFC 2 Yanga 1
Azam 1 Simba 2

mshikaji hapo juu, mbona unaleta unazi usio na manufaa dunia ya leo, kandambili ni kandambili

Anonymous said...

http://www.facebook.com/pages/I-am-a-FAN-of-YOUNG-AFRICANS-SC/144971678852174