Saturday, January 29, 2011

Kombe la Shirikisho Afrika

Yanga 4 Dedebit 4
Yanga leo imeanza kampeni yake ya jkuwania Kombe la Shirikisho Afrika kwa kusuasua baada ya kulazimishwa sare ya 4-4 kwenye Uwanja wa taifa Dar es Salaam.

Yanga ilikuwa ya kwanza kupat bao kupitia kwa Nadir Haroub lakini Wahabeshi hao walisawazisha na kuongeza mabao mengine mawili kabla ya Nurdin kuifungia Yanga bao la pili dakika chache kable ya mapumziko.

Katika kipindi cha pili Dedebit iliongeza bao la nne na wakati mashabiki wakiondoka uwanjani katika dakika za lala salama Godfrey Bonny aliisawazishia Yanga bao la nne.

8 comments:

Anonymous said...

hii drew ni ngumu sana ugenini tunatakiwa kushinda ili tuendelee vinginevyo tushatoka kila la kheri ktk marudiano

Anonymous said...

Tumemaliza mashindano, watu wamesajili usanii hela simeibiwa wanajaza au wanaadika mikataba ya uongo? Hela hizo tungekuwa na timu ya uhakika kama TP MAzembe

Anonymous said...

gogoro linaitafuna yanga,yanga inapita ktk uongozi mbovu ever,timua mwenyekiti na makamo wake ,na huyu manji nae kimeo pia lzm tujue hilo,hanatumia pesa zake kudidimiza yanga lzm tuamke na kujua hilo.

Anonymous said...

Acheni kumlaumu Manji, yeye katoa hela za usajili watu wanaandika mikataba ya uongo, katoa pesa kukarabati jengo, lakini halikurabatiwa vizuri kwa hela alizotoa, katoa pesa kila chumba kiwe na flat Tv, hawakununua zinazotakiwa. Sasa hapa anahujumu kweli?
Tuwe wa kweli huyu jamaa alivyokuwa amejipinda Yanga ingekuwa na uongozi mzuri sasa hivi wangekuwa wamefanya maajabu katika maendeleo

Anonymous said...

huyu hapo juu anamlaumu manji nafikiri aje kuifadhili yanga angalau kamilioni ,moja tuu labda tutaendelea.

Anonymous said...

matokeo vipi huko nyumbani mtibwa na yanga tujulisheni

Anonymous said...

Angalia www.yangasc.com. Kila dakika kuna update mpria mzima

Anonymous said...

Yanga 0 Mtibwa 1 mpira umekwisha