Saturday, May 26, 2012

Nchunga Ajiuzulu

Hatimaye Mwenyekiti wa Yanga mwanasheria Lloyd Nchunga ametangaza rasmi kujiuzulu nafasi yake hiyo aliyokuwa anaishikilia baada ya kulalamikiwa na wanachama wa klabu hiyo kuwa ameshindwa kuwangoza.

Shinikizo lililomsukuma Nchunga kuachia madaraka hayo lilionekana kuzidi pale wanachama zaidi ya 700 walioongozwa na Baraza la Wazee walipokutana kwenye makao makuu ya klabu hiyo Jumapili iliyopita katika mkutano wa wanachama ambao haukuwa rasmi kwa mujibu wa katiba.

Ufuatao ni waraka wa kutangaza kujiuzulu kwa Mwenyekiti Lloyd Nchunga.

Ndugu wana Habari,

Najua kwamba taarifa hii itawafedhehesha wajumbe na wanayanga wanaotuunga mkono,hasa ukizingatia maamuzi ya pamoja ya vikao vyetu vya kamati ya utendaji vilivyopita kwamba hakuna wa kujiuzulu kati yetu mpaka tujue hatma ya mkutano mkuu ambao tulipanga ufanyike tarehe 15 Julai 2012, ukiachia mbali shinikizo la kujiuzulu linalotolewa na baadhi ya wazee na wanaojiita vijana wa klabu, kwa wajumbe wa kamati ya utendaji, na hasa mimi kama mwenyekiti.

Nawashukuru wajumbe kwamba tulifanya kazi kwa pamoja na kwa ushirikiano mzuri, na hata pale tulipotofautiana tulifanya hivyo kwa hoja na kufikia maazimio ambayo wote tulikuwa tunawajibika nayo.

Tangu tumeingia madarakani tumeweza kushirikiana na kupata mataji matatu katika kipindi cha mwaka mmoja, yaani; Ngao ya Hisani 2010, Ubingwa wa ligi kuu ya Vodacom 2010/2011, na Ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup), 2011. Zaidi ni kwamba tuliuwa uteja kwa watani wetu wa jadi kila tulipokutana katika ligi ukiachia mbali mechi ya tarehe 6 Mei 2012, ambayo tulifungwa goli 5 bila, na kuleta mtafaruku mkubwa katika klabu yetu.

Hali kadhalika tumeshirikiana mpaka tumeweza kuboresha mkataba kati yetu na TBL kupitia Kilimanjaro Premium Lager, tumeingia mkataba na kampuni ya NEDCO kuendeleza mali zetu katika mtaa wa mafia na uwanja wetu wa KAUNDA baada ya kufikia hatua nzuri katika kupata hati miliki za maeneo yote mawili.

Nafahamu kwamba kampuni hiyo iko katika hatua za mwisho za kumalizia michoro. Hali kadhalika tuliingia mkataba wa kuzalisha na kuuza bidhaa zenye nembo yetu na hasa baada ya kufanya marekebisho yatokanayo na matakwa ya sheria kule BRELA na pia mkataba na kampuni ya NEXUS LTD, ambayo itakuwa inatutafutia wadhamini wa nje na ndani, kufanya promosheni zetu na kampeni kwa njia ya electronic kupitia mitandao mbalimbali na kukusanya data za wanachama na kusajili wapya tukiwa na malengo ya kukusanya shilingi 300,000,000/= hadi 800,000,000/= kwa mwaka katika kipindi cha miaka mitatu. Haya yote tuliyafanya tukilenga kujitegemea kujazia mapengo yaliyokuwa yakitokana na kutegemea ufadhili wa mtu mmoja mmoja.

Kwa ridhaa yenu tumekua tukiendelea na mazungumzo na makampuni mbali mbali kwa ajili ya udhamini na kwa sababu maalum, nitazitaja katika hati ya makabidhiano kwa kiongozi ajaye.

Aidha, tumeshirikiana katika kufanya mambo mbali mbali ya kijamii, ikiwa ni pamoja na sikukuu ya kuadhimisha miaka 77 ya Yanga, sikukuu za pasaka, kuchangia jamii na waliokumbwa na maafa, na kongamano la vijana lililolenga kuwaamsha vijana kuitambua nafasi yao katika Yanga ikiwa ni pamoja na kupata azimio la kuanzisha SACCOSS ya Yanga, ambapo maombi yapo kwa msajili Manispaa ya Ilala.

Haya yote nayataja ikiwa ni kuwashukuru kwa ushirikiano na ikiwezekana muweze kuyakamilisha yaliyobaki ambayo mtaona yalikuwa mazuri. Lakini pia tulipopata matatizo tulikuwa pamoja. Nichelee kusema tu kwamba tulisimama pamoja baada ya kujiuzulu Makamu Mwenyekiti wetu Ndugu Davis Mosha na mjumbe wetu ndugu Seif A. Seif, Ali Mayayi, na wengineo, kwani tulifungwa na katiba.Tulisimama pamoja pia katika suala la kujiuzulu ndugu Yusuf M. Manji, aliyekuwa mdhamini mteule na mfadhili mkuu ambaye sasa ameonyesha nia ya kurudi nanyi mkaridhia mkutane naye.

Awali, tulitumia kila jitihada za kumrejesha lakini ikashindikana. Hata hivyo doa limetupata baada ya kufungwa na watani wetu goli 5 bila, ambapo kuna wanachama wanaoelewa na wasioelewa kabisa.

Ninachokiona mimi ni usaliti wa hali ya juu uliombatana na matukio mbalimbali yaliyopita na yanayoendelea hadi kujaribu kupindua uongozi wa halali wa kidemokrasia. SIWATUHUMU WACHEZAJI MOJA KWA MOJA, isipokuwa mfululizo wa matukio wiki tatu kabla ya mchezo ule na sasa, inaonyesha kwamba kulikuwa na usaliti mkubwa ambao sisi hatukuweza kuubaini mapema. Sioni mantiki katika hoja kwamba wachezaji walikuwa wakidai mishahara, posho n.k. Au ati mtendaji wetu alishikiliwa Arusha kwa deni la hoteli, ndiyo tuvune bao 5!

Kwa wanaoijua Yanga, imewahi kuwa na madeni makubwa katika Hoteli mbali mbali, mawakala wa ndege n.k, na baadhi tumeyakuta na sisi tumekuja tukayalipa. Hii imewahi kutokea kabla na wakati akiwepo mfadhili, sembuse sisi tulioachwa baki, na bado wachezaji walicheza kwa morali.

Hata hivyo, utamaduni wa kutimuana baada ya matokeo mabaya ni dhambi ambayo itatula kama hatutaiacha, kwani wenye hila na uchu wa madaraka wataendelea kutumia mbinu hiyo ili kuuondoa uongozi wa kidemokrasia. Baada ya mapinduzi kushindikana na TFF kuonya kuhusu mapinduzi hayo, wazee kupitia msemaji wao , Mzee Akilimali wamesikika katika kipindi cha Michezo cha Redio moja maarufu hapa nchini wakidai kwamba ni bora Yanga ishushwe daraja au kufungiwa kuliko mimi kuendelea kuongoza! Hii imenikumbusha HEKMA ZA MFALME SELEMANI akiamulia ugomvi wa wanawake wawili waliokuwa wakigombea mtoto naye akaamuru wamgawane nusu kwa nusu. Yule mwenye mtoto kweli alimuomba Mfalme amuachie mwenzie kuliko kumkata nusu. Kwa hekma hiyo nimeamua kujiuzulu nafasi yangu katika Uenyekiti wa Yanga kwani ni klab ninayoipenda hata kama sio kiongozi kwa mujibu wa ibara ya 28 ya katiba yetu.

Vile vile siko tayari kuona klab yangu ikisalitiwa au kuhujumiwa eti kwa sababu tu mimi ni kiongozi. Natumaini kamati ya utendaji kwa pamoja na wale tuliowateua chini ya ibara ya 29(3) ya katiba ya Yanga pamoja na bodi ya wadhamini, itawaongoza wanachama mpaka kufikia mkutano mkuu kwa mafanikio zaidi.

Nitaendelea kuwa mwanachama mwadilifu na nitatoa mchango wangu wa hali na mali pale nitakapo hitajika na nikiwa na uwezo wa kufanya hivyo.

YANGA DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO.

Wasalaam,

LLOYD NCHUNGA BIHARAGU.

Nakala kwa:-
Mama Fatma Karume,
Mdhamini Francis Kifukwe,
Mdhamini Bwana Yusuf Manji – Kwa taarifa

LLOYD NCHUNGA BIHARAGU
C/O LLOYD ADVOCATES,
Morogoro/Bibi TIti Mohamed Rd,
7th Floor, J.K. Nyerere Pension towers
P.O. BOX 75111,
Dar-Es- Salaam,
Tanzania.



6 comments:

Anonymous said...

ciqs [url=http://www.bootswould.com]uggs boots sale[/url]
Following your Westchester Squad eventually left, I acquired to interview he herself Kobe Dez bryant. I do believe Specialists the issue that a majority of any supporter of Kobes shoes or boots will be grateful for. Happily, We have this Q A on Online video media and putting up it as a follow-up to this particular submit. Potential predators anyone?! The one thing I'd been very happy to hear is this fact yr we convey more of the true to dimension basketball game overall performance footwear. Seems as if We are catching personally each and every pair this Animalistic Calendar year of the Kobe VII. Do not miss out! Stay Tuned In As Usual - LAKER Bad guy


gpvm [url=http://www.bootssay.com]ugg boots outlet store[/url]
So the day's the test Klaus and Violet passed there just be sure you Sun-drenched had done stapling the forms Mister. Nero had told her to do. So they really all got to stay the school. Instructor Genghis decided not to like this. Then he ended up searching for the problem twin babies accomplishing the moment to the a few and Olaf fount out in regards to the boy twins using a fortune and then he leaped way while using twins babies. But ultimately he lastly uncovers themself..


fgoz [url=http://www.bootssay.com]www.bootssay.com[/url]
So why america can be China's initially airplanes service to exhibit such concern about it? Because they on their own stated, or China's armed forces transparency hesitant, he uses a Inchbattle mentality" as opposed to Intranquil thoughtsIn to observe China's each and every shift, this battle is a feeling of thinking proper setting of his own nation and armed forces judgement! These and China's tranquil increase of nationwide identity are incompatible, which is hard to accomplish good believe in. would like Cina to build a healthy and dependable armed forces interaction, but the utilization of avenues to China's progress suspicious, which means that China's progress, said the carrier's motive should you not recognize, it truly is not possible to possess a healthful armed forces interaction of communal have faith in. These True UGG Boots will fly off the shelves when the 1st snowflake of the season struck the bottom. The only real is constructed of Avoi - a gum rubberized only which blankets your foot or so if you stroll.

Anonymous said...

Even if hе rеcοmmеnds yοu some that aге
highly effective, but lоng-term use for wеight
lоss and аs a toρiсal ointmеnt.

You will find that yοu sрend lots οf cаѕh and risκ thеiг phyѕіcal condition.

Theге aгe pure green cоffee bean extract
800 mg thаt cаn be fаtal or tаke
a pгeѕcriptiοn? It cοmes ԁown іn the stоmach so
you will eat less just becаuse your boԁy does not make ѕеnsе to ovеr indulgе with
the ωrong foods.

Also visit my wеblog pure green coffee extract

Dewi said...

Nice blog.

Een Irawati said...

please go http://eenirawati81.blogspot.com/

privat yuk lampung said...

thanks for share..
Privat Yuk Lampung | Mahan Guru Lampung

Unknown said...

visit me back :)
Thanks