Sunday, July 13, 2008

Mtihani wa kwanza leo

BAADA ya jana kuishuhudia Simba ikilizwa mabao 3-2 na Tusker ya Kenya, leo ni zamu ya Yanga kuwakabili mabingwa watetezi, APR ya Rwanda katika mchezo wa Kundi C utakaofanyika kwenye Uwanja Mkuu wa Taifa.


Yanga, ikiwa na silaha zake zilizoandaliwa mahsusi kwa michuano hiyo na ile ya kimataifa itaingia kwenye uwanja kwa tahadhari kubwa. Golini anatarajiwa kuwa Juma Kaseja ambaye atalindwa na ngome itakayoongozwa na Wisdom Ndhlovu na George Owino. Bila shaka katika ushambuliaji kutakuwa na kazi kubwa katika upangaji kwani Yanga kwa sasa ina washambuliaji wengi walio katika hali nzuri ya kimchezo.


Yanga, ambayo katika michezo ya kujinoa iliilaza Express ya Uganda kwa bao 1-0 na pia kuizima Mbagala Market kwa mabao 2-0, inabeba jukumu la kuanza vizuri ili kurejea imani ya mashabiki wake na Watanzania.


Lakini, Yanga inatarajia upinzani mkali kutoka kwa vijana wa APR, ambayo kwa sasa inanolewa na Mholanzi Renne Feller na inajivunia mshambuliaji wao hatari Haruna Niyonzima.


APR, ambao ni mabingwa watetezi wa michuano hii waliwasili nchini wakidai kuwa wametumwa na Rais Kagame warejee Kigali na kombe hilo.

Tusubiri tuone hizo dk 90 .

7 comments:

Anonymous said...

Mkuu tupe matokeo na tathmini ya mechi ya APR

Anonymous said...

bado mapema hata mechi haijaanza, labda atupe line up ikoje?

Anonymous said...

vipi huko

Anonymous said...

Naji ya shingo.

Anonymous said...

MAJI

Anonymous said...

Jamani tuambieni kinachoendelea, hayo maneno ya maji ya shingo hayasaidii

Anonymous said...

APR 2 Yanga 2