Wednesday, October 29, 2008

Hii ni Offside?
Picha kutoka Mwanaspoti
Kuna habari kwamba goli pekee la Yanga katika mchezo dhidi ya Simba halikuwa halali kwa vile mfungaji - Ben Mwalala wakati anapokea pasi kutoka kwa Boniface Ambani alikuwa tayari ameotea (offside). Pichani ni wakati Ambani anatoa pasi kwa Mwalala. Je, hii ni offside? Naomba mawazo yenu.

15 comments:

Anonymous said...

Inaonekana clear kabisa hapo Mwalala hayupo offside kwa vile mchezaji wa Simba aliyeanguka yupo katika usawa mmoja (parallel) naye.

Mie naona hilo ni goli safi tu.

Anonymous said...

hilo ni goli tu amna offside apo anaesema ni offside basi ujue yeye ni simba ambao bado wanataptapa maana wameshakufa maji aho!!!!

MARTIN PAULO SINGANO said...

hilo ni goli tu amna offside apo anaesema ni offside basi ujue yeye ni simba ambao bado wanatapatapa maana wameshakufa maji aho!!!!

MARTIN PAULO SINGANO said...

hilo ni goli tu zuri hata ukampa refa aliechezesha mechi ya fainali ya kombe la dunia mwaka 2006 kati ya italy na france atalikubali tu kuwa ni goli!!!!

Anonymous said...

Vichaa ndiyo watakaoseme ni offside..

Anonymous said...

Simba wananishangaza sana hirizi waweke wenye halafu baadaye wanaikataa wenyewe baada ya kusahau kuihamisha... dhanu huyo Dalali wao atafungiwa kesho wa ushirikina wake na mwanga msaidizi Mgosi.

MARTIN PAULO SINGANO said...

Wamekwisha hao hawana lolote na mwaka huu wasipo angalia watashuka daraja wanatakiwa wakaze buti

Sisi wana YANGA tuna songa mbele tu!!!!!!

John Mwaipopo said...

tena muwakumbushe simba hapo Ben Mwalala alikuwa katika kasi ya ajabu akitokea nyuma.hata kama kulikuwa na offside (ambayo haikuwepo) haikumhusu mwalala kwa kuwa alikuwa akitoka nyuma kwa kasi ya kufa mtu. hao sokwe, sorry simba, walie tu mwaka huu.

John Mwaipopo said...

Wazee picha zingine ziko kwangu nitembeleeni

Anonymous said...

1. sio offside.
huyo beki anayemkaba ambani yuko level na mwalala, na ikumbukwe hii picha imepigwa muda mchache (in micro-seconds) baada ya ambani kuugusa/kupiga mpira kwa hiyo kuna 'movement' ime-take place ktk kipindi hicho kifupi na hivyo wengine kufikiria mambo ya offside.
Au kwa maneno mengine: Hao wachezaji wote watatu wako ktk 'motion' na mpiga mpicha alichelewa kupiga picha wakati ambani anatuma pasi (picha inaonyesha tayari ameshapiga mpira)!

2. kamera 'angle' haiko sambamba na mstari wa eneo la hatari (18) (penalty area) na hivyo kudanganya watazamaji wa hii picha na kudhani kuwa mwalala amezidi.

Anonymous said...

Inconclussive. Inaweka ikawa ni offside - inawezekana Ambani ndiye aliyekuwa offside wakati anapokea mpira. Ila tumeshashida. Historia itabaki Yanga 1 Simba 0

Anonymous said...

How comes Ambani awe offside wakati aliambaa na mpira kuanzia katikati ya uwanja upande wa mashariki?

Anonymous said...

SIMBA WAPUUZI. TATIZO NI KUPANIA KUIUNGA YANGA BADALA YA KUTAFUTA UBINGWA. MBONA WADOGO ZETU TOTO WAMEWACHAPA NNE MOJA LAKINI KIMYA SISI KUWACHAPA WANAONA AJABU KAMA MWANAUME KUPIGWA NA MKEWE. SIMBA ACHENI UJINGA TUMESHAWAFUNGA BASI KUBALINI. MBONA SIE WASTAARABU TU? MIAKA MINANE YOTE MNATUFUNGA TUNADROO SISI KIMYA TUU. NYIE KUFUNGWA INAKUWA ISSSUE? KWELI MTOTO UKIMZOEZA CHOCOLATE SIKU UNAMPOMPA BOGA NI TATIZO. YANGA OYEEEEEEEEEEE.

Anonymous said...

mwaipopo, ndaga fijo kwa picha kwenye blog yako. Kama unazo nyingine naomba utuwekee. Wazee mechi ya kesho vipi kutu kila mechi ina umuhimu sana. Mzee CM hauendi Moro?

Anonymous said...

its offside but kwa lines man kuona ni tabu sana sababu ni kiatu tu ndo kilozidi ..maradona kafunga la mkono na lilikuwa goal kama offsside basi hili ni offside lkn kama goal hili ni goal yanga oyeee