Thursday, June 18, 2009

TFF vs Yanga

Vuta nikuvute
Shirikisho la soka nchini (TFF) limelimesema baada ya klabu ya Yanga kushindwa kuwasilisha orodha ya wachezaji iliyowaacha kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, inatambua klabu hiyo haijaacha mchezaji yeyote msimu huu. Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam jana na Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela wakati akizungumzia suala la usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao, ambapo juzi ilikuwa mwisho wa kuwasilisha majina ya wachezaji walioachwa.

Kwa habari kamili cheki hapa.

6 comments:

Anonymous said...

I'm pleased to air my views on this issue,the way i see it is a normal dubious way of working TFF are used to.
Back from Fifa Congress Two weeks ago, TFF presida Tenga was quoted by press saying all U-20 players will be allowed to play in premier league, thats good, but the regulations allowing tha are not there!!!!!
The same applies to the matter at hand, TFF is doing its activities esp on players' registration without the regulations.

The last year's regulations seazed after the end of last year's season.

I join hands with our leaders to challenge them on their (TFF'S) primitive ways of running their issues.

it is time we say no to Ubabaishaji.

lakini wakubwa, usajili wetu umetulia????
tusijejikita kwenye hoja hii wakati mambo yetu shaghalabagala.

Nawasilisha

Anonymous said...

Mimi ni Yanga damu kam wengine hapo. Kwa ukweli ulivyo hatuna fedha ya kusajili, Manji amekataa kutoa fedha walizokuwa wanataka, hali ndiyo hiyo. Manji amesema lengo lilikuwa ni kusajili timu nzuri msimu uliopita, halafu kuuza wachezaji na fedha zitakazopatikana zingetumika kununulia wachezaji, kwa hili limeshindikana, na yeye amesema hawezi kutoa Million 200 viongozi walizoomba kwaajili ya usajili. Hata jana kulikuwa na kikao cha muda mrefu kati ya Manji na viongozi....tungoje tuone

Anonymous said...

mh yanga jamaniiiiiii,tusijepata aibuu,mimi naipenda sanaa hii timu tusichanganyikiwe kwa kuondoka kwa kaseja jamani huwenda ametuepushia mengi na hivyo mtu mwenyewe naskikia ana kadi ya msimbzi duh! angeuza timu wadau kama ingewezekana wangeanzisha mfuko wa kuisaidia timu kama wenzao simba lakini kwa sasa ni too late ila tusikate tamaa simba si lolote maneno tu yale,wanaongea sanaaaaaa lakini utekelezaji ni mdogo tusiwaogope.Tina

MASEBE said...

MZEE CM KUNA NINI,HEBU TUJULISHE HABARI ZA HAKIKA ZA USAJILIWETU,UMEKUWA KIMYA MNO,UWANJA SASA UMEPOA KABISA,TUNAHITAJI HABARI MPYA.USAJILI WETU VIPI? WAKUACHWA NAO IMEKAAJE, HEBU LETE HABARI WEWE UKO JIKONI, SIYE WENGINE TUKO KIJIJINI

Anonymous said...

Tumefulia.Kutegemea mtu mmoja sasa ameanza kuturingia.Madega naye hana njia mbadala.Tumekwama tunabaki kubembeleza.Aibu tupu.

Anonymous said...

Sasa haya mliyoandakia, sasa hela zimetoka wapi? hebu achane mambo ya kitoto ohh mimi nina habari toka ndani Mani kakataa kutoa pesa au nyin yi ndo mamluki wa Simba nini?