Wednesday, June 17, 2009

USAJILI 2009/10

Nondo zote kwa Kondic

Suala usajili wa klabu ya Yanga kwa msimu ujao safari hii limekuwa la tofauti sana kutokana na klabu hiyo kukabidhi nondo zote kushughulikiwa na Kocha Dusan Kondic.

Mchezaji pekee ambaye kwa uhakika ametangazwa kusajiliwa na klabu nyingine ni kiungo Castory Mumbara ambaye amejiunga na timu iliyopanda daraja ya African Lyon ya Dar es Salaam. Soma hapa

Juzi Yanga ilitakiwa kuwasilisha TFF majina ya wachezaji itakaowaacha kwa msimu ujao laikini haikufanya hivyo kutokana na kudai kwamba hawaandikiwa barua na TFF kuhusu suala hilo.

TFF kwa upande wake imeikabidhi Yanga barua hiyo jana.

Hata hivyo baadhi ya vyanzo vya habari vinadai kwamba Yanga ilishindwa kuwasilisha majina hayo kwa vile Kondic ambaye ndiye mwenye majina hayo hayupo nchini kwa sasa.

Tutazidi kujulishana yanayojiri.

1 comment:

Anonymous said...

duh mheshimiwa mbona unatuchelewesha kutupa stori za yanga jamani! mimi ni mdau kila siku nafungua hii website lakini naona hamna updates news ehee mdau mdau.ila mimi ninaomba kuuliza kuna gazeti nilisoma wameandika ambani anakuja kuendeleza historia yake yanga,sasa nauliza ambani anarudi aynaga au bado ana ndoto za kwenda china? naomba nisaidiwe jamani?.tina