Saturday, August 29, 2009

Ligi Kuu ya Vodacom

Kivumbi kuendelea leo

Ligi Kuu ya Vodacom inaendelea tena leo kwa mechi tatu kwa ambapo Yanga itaingia katika Uwanja wa Uhuru kupambana na timu iliyopanda daraja ya Manyema Rangers (Mkuki wa sumu).

Mechi nyingine itakuwa huko Mbeya ambapo Simba itashuka kwenye Uwanja wa Sokoine mjini humo kupambana na Prison ya huko.

Aidha Majimaji nayo itaikaribisha JKT Ruvu.

14 comments:

CM said...

Ni mapumziko Yanga 2 Manyema 0

CM said...

mabao ya Yanga yamefungwa na Vicent Barnabas na Mike Baraza

Anonymous said...

Matokeo ya viwanja vingine vipi CM

Anonymous said...

Mbeya Simba Lunyasi anaongoza kwa mabao matatu (3) kwa nunge. Wafungaji ni Mgosi (2) na Boban

Anonymous said...

matokeo bado mapumziko

Anonymous said...

haya Manyema wamerudisha, game ni 2-2. Simba kashinda 4-0

Anonymous said...

Wadau acheni uzushi. Yanga wametandika mtu tatu, bao mbili za Tegete. Simba walikuwa wanaongoza moja hadi dakika ya 75.

Anonymous said...

Sasa kama alikuwa anaongoza kwa bao moja hadi dk ya 75 ina maana hawezi kufunga goli 3 ndani ya dk 15?

Anonymous said...

Jamani mbona mnatupa habari za kutatanisha? CM Said tupe news wewe mimi nakuaminia zaidi, naona hawa omba omba wameanza kuingia kwenye blog yetu

CM said...

matokeo ya mechi za leo:
Yanga 3 Manyema 0
Prisons 0 Simba 1
Majimaji 0 JKT 1

Anonymous said...

simba anaweza kumfunga 4 prison lakini wachezaji wote wa simba wanatakiwa wawe na miguu mitatu mitatu si unajua mwanasimba mwezetu.....hebu kua na akili unaandika kwenye blog hii panya wewe.

Anonymous said...

mayanga mkae tayari kufungwa na simba mtakoma

Anonymous said...

Anonymous wa Aug 29, 2009 7:07:00 PM Simba hawawezi kuwafunga Prisons mabao matatu katika dakika 15 za mwisho huko Mbeya. Matokeo ya mwisho yamedhihirisha hilo.
Unawatia aibu Simba wenzio.

Anonymous said...

Mtajiju!!!!!!!