Saturday, December 26, 2009

Muuaji wa mnyama

Mchezaji wa Yanga Shamte Ally ambaye amepeleka huzuni kubwa mtaa wa Msimbazi kwa kupachika bao la ushindi la timu yake dhidi ya Simba katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la Tusker. Yanga ilishinda 2-1.

8 comments:

Anonymous said...

Kwa stahili ile ya uchezaji na spirit ya wachezaji ilivyo kama itaendelea basi kwa miaka kama mitatu ijayo yanga itakuwa ni balaa.
Sina budi kumpongwza mwalimu kwa mfumo anaoutumia kwa kutoa kipaumbele kwa wachezaji wazawa na kuachana na hawa watalii wanaokuja kutuchuna tu.
Namshauri Manji aache kudanganywa na wapenda cha juu kwa kutuletea wachezaji ambao hawana tija yoyote kutoka nje. Kama yuko serious basi ahakikishe hiki kikosi kinabaki muda mrefu sio siri combination ya Ngassa,Tegete, Kigi ikikaa pamoja kwa muda itakuwa ni balaa.

Anonymous said...

ndugu zangu niko mbali hili jinyama nasikia limeumia tena kweli? kama kweli dua zangu nzuri simuombei dua nzuri maisha mnyama.

CM said...

Simba imejifariji kwa ushindi wa tatu leo baada ya kuwafunga wachovu Tuker FC 2-1

Anonymous said...

asante cm ,kama tumelinyoa misharubu jinyama, huyo paka dawa yake samaki, asubiri kibondo.

Anonymous said...

CM, vipi Manji amekubali kugombea uenyekiti Yanga au amewatolea wazee nje? tupeni habari basi.

Anonymous said...

cm usiwe mbali kutuhabarisha kuhusu kibondo cha PAKA thnx!

Anonymous said...

paka analia nimemwambia akamsadie simba

Unknown said...

Paka kapigwa 2-1, Manji amekataa kugombea uenyekiti na pia kaandika barua kwa wazee kujitoa ufadhili. Ingawa Madega kakanusha akidai uongozi haujapata barua ya kujitoa kwake na kumwaga lawama kwa wazee kwamba wanaleta chokochoko.