Tuesday, February 02, 2010

Yanga yaomba kuahirisha mechi

Mabingwa wa soka nchini, Yanga, wameliandikia barua shirikisho la soka nchini, TFF, kuomba kusogezwa mbele kwa mechi yao ya Jumatatu ijayo dhidi ya Mtibwa ili ipate nafasi ya kufanya maandalizi ya mchezo wao wa Ligi ya Klabu Bingwa Afrika dhidi ya FC Saint Eloi Lupopo ya DRC utakaofanyika Februari 13.


Afisa Habari wa klabu , Luis Sendeu, alisema kuwa barua hiyo imepelekwa jana TFF na wameomba mechi hiyo dhidi ya Mtibwa ipangiwe tarehe nyingine yoyote baada ya kufanyika kwa mchezo huo wa klabu bingwa.


Aidha, Sendeu alisema timu hiyo imekosa mechi za kimataifa za kirafiki za kujiandaa na Ligi ya Klabu Bingwa kutokana na maombi wanayoyatuma kugonga mwamba kila mahala kutokana na nchi nyingi kuwa bado zinaendela na ligi kuu zao.

No comments: