Thursday, May 13, 2010

Maftah amwangushia jumba bovu Nyoso

Hatimaye Amir Maftah ameujibu uongozi wa klabu ya Yanga kwamba kutolewa kwake kwa kadi nyekundu katika mechi dhidi ya Simba kulitokana na hasira za kutemewa mate na kuingo wa Simba Juma Nyoso.

Akihokiwa na kipindi cha michezo cha Times FM, Maftah alisema Nyoso alimtemea mate kwa maksudi ili apandishe hasira jambo ambalo alifanikiwa. Kutokana na hasira hizo, Maftah alimpiga kichwa Nyoso na kutolewa kwa kadi nyekundu.

AIdha Maftah amesema kitendo chake cha kutolewa kwa kadi nyekundu ni cha kawaida na amewaomba msamaha mashabiki wa Yanga kutokana na kitendo hicho.

Wakati huo huo mchezaji Nyoso naye alihojiwa kwa njia ya simu katika kipindi hicho na kudai kwamba hakumfanya lolote Maftah.

4 comments:

Anonymous said...

picha za video kama zilichukuliwa vizuri zitaonyesha ukweli kwa kurudiarudia.Lkn huwezi kusema tuangalie picha za television(video) ambazo huchukuliwa upande mmoja na wkt mwingine kuruka matukio.

Anonymous said...

tumsamehe maftah alipotea tuu.

Anonymous said...

ni kweli naunga mkono wazo lako kuwa tumsamehe ili tuanze usajili.Kuna hatari tukaupoteza tena ubingwa msimu ujao kama hatutajipanga vizuri maana leo nimesoma gazeti Enyimba tayari wameshamchukua mchezaji ambae tunategemea kumtumia msimu ujao wkt huo sisi tumeng`ang`ania Maftah alihujumu.NAOMBA TUJIPANGE KWAJILI YA MSIMU UJAO NA MICHEZO YA KIMATAIFA.MWALUSAKO NA TIMU YAKO MNAOBAKI TUNAOMBA MUWE MAKINI NA HILI

Anonymous said...

ni kweli naunga mkono wazo lako kuwa tumsamehe ili tuanze usajili.Kuna hatari tukaupoteza tena ubingwa msimu ujao kama hatutajipanga vizuri maana leo nimesoma gazeti Enyimba tayari wameshamchukua mchezaji ambae tunategemea kumtumia msimu ujao wkt huo sisi tumeng`ang`ania Maftah alihujumu.NAOMBA TUJIPANGE KWAJILI YA MSIMU UJAO NA MICHEZO YA KIMATAIFA.MWALUSAKO NA TIMU YAKO MNAOBAKI TUNAOMBA MUWE MAKINI NA HILI