Saturday, July 17, 2010

Uchaguzi Mkuu huoo

Hatimaye siku ya uchaguzi mkuu wa klabu ya Yanga imefika ambapo wanachama wa klabu hiyo watapiga kura (Julai 18) katika ukumbi wa PTA Sabasaba kuchagua viongozi wapya.

Wanaowania nafasi hizo ni kama ifuatavyo:

Mwenyekiti
1. Lloyd Nchunga
2. Abeid Abeid
3. Edgar Chibura
4. Mbaraka Igangula
5. Francis Kifukwe

Makamu wa Mwenyekiti
1. Davis Mosha
2. Constatine Maligo


Wajumbe wa kamati ya Utendaji
Yusuf Yasin, Robert Kasela, Shaban Mohamed, Omary Ndula, Atufwigwegwe Mwakatumbula, Evance Matee, David Peter, Majid Simba, Mzee Yusuf, Ramadhan Kampira, Edgar Fongo, Jackson Maagi, Mwinyi Mangara, Hamis Ambari na Mohamed Bhinda.

Wengine ni Isaac Mazwile, Paul Malume, Sarah Ramadhan, Salim Rupia, Dk. David Luhago, Titto Ossoro, Charles Mugondo, Ally Mayay, Pascal Kihanga, Ismail Idrissa, Lameck Nyambaya, John Mayala, Theonest Rutashoborwa na George Manyama.

Tunawatakia uchaguzi mwema

6 comments:

Anonymous said...

Kifukwe amejitoa kugombea Uenyekiti kutokana na hotuba za ufunguzi wa mkutano huo wa uchaguzi kuonekana kumlenga kumharibia.

Anonymous said...

Mdhamini wa Yanga ametoa sharti kwa wagombea uenyekiti wa klabu hiyo kwamba atakayeshinda kiti hicho ni lazima amteue Francis Kifukwe kuwa mdamini mwenzake vinginevyo naye ataipa kisogo klabu hiyo.

Anonymous said...

what is going on?

Anonymous said...

mambo yamekuwa mambo, kuku kujamba msibani ha ha ha

Anonymous said...

aibu si aibu babu ,ndio wanasema mtu ukimzuia riziki atavua hata nguo.

Anonymous said...

Yamepita,tujipange kwa ajili ya kuangalia yaliyo mbele yetu.Utakuwa si Yanga wa kweli kama utaihujumu klabu eti kwakuwa Kifukwe hakuchaguliwa.Yanga ilikuwepo kabla ya KIfukwe na wote waliogombea hawajazaliwa.Unaipenda Yanga kama klabu au wapenda viongozi!acha hizo. Viongozi ni watu wa kupita tu. Tuipende timu yetu, tuwape moyo walio tayari kuisaidia kwa nia nzuri nasi tuwe wakweli kwa klabu.