Wednesday, July 14, 2010

Uchaguzi wa Yanga

Nyenzi ajitoa

Mgombea wa nafasi ya Umakamu wa Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Ayoub Nyenzi amejitoa kuwania nafasi hiyo katika kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu wa klabu utakaofanyika Julai 18.

Kujitoa kwa Nyenzi kunaiacha nafasi hiyo kugombewa na watu wawili Davis Mosha na Constantine Maligo.

Ayubu Nyenzi amejitoa kwenye kinyang’anyiro hicho kwa madai ya sera zake na za baadhi ya wagombea mwenzake wa nafasi hiyo zinafanana. Mgombea mwenzake aliyetajwa kufanana sera ni Davis Mosha.

Kampeni za uchaguzi huo ambambao utafanyika Jumapili bado zinaendelea.

No comments: