Monday, August 23, 2010

Constantine Maligo afariki
Aliyewahi kuwa katibu mkuu msaidizi wa klabu ya Yanga Constantine Maligo amefariki dunia.

Mwili wa marehemu Maligo ambaye aliingia madarakani chini ya uongozi wa Rashid Ngozoma Matunda mwaka 1996 umeagwa leo nyumbani kwake huko Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Marehemu Maligo aliwahi pia kugombea nafasi ya Ukatibu mkuu mwaka 2007 lakini akashindwa na Lucas Kisasa na mwezi uliopita alishindwa katika nafasi ya Umakamu wa mwenyekiti ambayo ilichukuliwa na Davis Mosha.

Mungu ailaze mahali pema roho ya Marehemu Constantine Maligo.

3 comments:

Anonymous said...

Poleni sana familia, ndugu, jamaa na wana-Yanga wenzangu wote kwa ujumla kwa msiba wa mwenzetu, mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi. Amen.

Anonymous said...

Kwa niaba ya familiya ya Zellahs, napenda kutoa pole zangu za huzuni kubwa kwa kifo cha Ndugu yetu mpendwa Constantine Maligo. Nasikitika sana kwani Maligo nilisoma naye pale ATC hadi 1989 na alikuwa kijana mkalimu, chapakazi na mwenye afya nzuri na mawazo ya kisasa. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi. Amina.

julius Zellah

Anonymous said...

Wajameni,

Ile website tuliyotangaziwa kuwa inajengwa , vipi imefikia wapi? maana ni karibu mwaka wa pili unaingia na ni kimia kabisa