Mtihani wa Pan Africa
Pan Africa kwa sasa inaburuza mkia wa ligi hiyo kwani hadi sasa ina pointi 4 tu katika michezo 8 iliyocheza hadi sasa. Nayo Yanga itataka kutumia mechi hiyo kushinda ili kujijengea kujiamini kabla ya pambano lake dhidi ya Simba Jumatano wiki ijayo.
Kwa kweli ushindi ni muhimu kwa vijana wetu ambao katika mechi yao ya mwisho walicheza chini ya kiwango kiasi cha kulazimishwa sare ya 0-0 na vijana wa Moro United.
Kwa wale wanaopendelea kufuatilia kinachoendelea ndani ya dakika 90 za mchezo, kama desturi yetu mnaweza kupita hapa chini katika comments.
6 comments:
Hadi sasa ni mapumziko bado ni 0-0.
Asante kwa latest hizi. Endelea na moyo huu! Kila la heri Yanga!
tupo wote tuletee habari man
Full time 0-0
Mwalala amefungiwa mechi 6. Sijui tutatoka vipi J5?
Fitina za msimbazi hizo, lakini tutatoka tuu. Makocha na viongozi washughulikie suala na nidhamu, saabu kadi zingine wachezaji wanapata sii za lazima.
Post a Comment