TAIFA STARS SPECIAL
Tutawatoa Uganda Cranes leo?
Tutawatoa Uganda Cranes leo?
Timu ya Taifa ya soka ya Tanzania Taifa Stars leo inajitupa katika Uwanja wa Nakivubo huko Kampala Uganda kuchuana na Timu ya Taifa ya nchi hiyo - Uganda Cranes katika mchezo wa marudiano wa Kombe la Afrika kwa wachezaji wa ndani ya nchi (CHAN).
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika wiki 2 zilizopita huko Mwanza, Taifa Stars ilishinda 2-0 hivyo leo Cranes wanahitaji ushindi wa kuanzia 3-0 ili isonge mbele. Mshindi wa raundi hii huenda akakutana na Sudan ambayo iliifunga Rwanda 4-0 katika mchezo wa awali huko Khartoum wiki mbili zilizopita. Fainali za michuano hiyo zimepangwa kufanyika mapema mwakani huko Ivory Coast
Tunawatakia kila la heri vijana wetu huko Kampala, licha ya vituko vya mwaka 47 walivyofanyiwa na wenyeji wetu huko. Kama kawaida mnaweza kufuatilia mtanange huu katika comments hapo chini ili kujua kinachoendelea katika dakika 90 za mchezo.
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika wiki 2 zilizopita huko Mwanza, Taifa Stars ilishinda 2-0 hivyo leo Cranes wanahitaji ushindi wa kuanzia 3-0 ili isonge mbele. Mshindi wa raundi hii huenda akakutana na Sudan ambayo iliifunga Rwanda 4-0 katika mchezo wa awali huko Khartoum wiki mbili zilizopita. Fainali za michuano hiyo zimepangwa kufanyika mapema mwakani huko Ivory Coast
Tunawatakia kila la heri vijana wetu huko Kampala, licha ya vituko vya mwaka 47 walivyofanyiwa na wenyeji wetu huko. Kama kawaida mnaweza kufuatilia mtanange huu katika comments hapo chini ili kujua kinachoendelea katika dakika 90 za mchezo.
11 comments:
mpira unakaribia mapumziko, tupo nyuma kwa bao moja.
matokeo vipi? kipindi cha pili kishaanza
vipi list yetu ikoje?
Ngapi ngapi mazeee mpira haujaisha tu
BADO NI 1-1. NI DAKIKA YA 88 SASA
mpira umekwisha, tumefanikiwa kuwatoa Uganda Cranes kwa jumla ya 3-1.(2-0), (1-1)
Big up sana tanzania soccer sasa linatia matumaini, Kazi imebaki moja kuwakabali Sudan
hongera vijana wa stars mbele kwa mbele uzi huo huo uliomtoa kenya na uganda uwatoe wasudan hongera kwa wa tanzania woooooooote
m sakran kuwait
yeeeeeeh
TZ tuna faida kubwa kwa kuwa vijana wetu wote wanacheza soka nyumbani, hivyo ni rahisi kuwakabili kina Ghana, Nigeria, Ivory Coast n.k kwa vile vikosi vyao hutegemea sana 'oxygen' kutoka ulaya!!
tusiwadharau hata kidogo.
Post a Comment