Thursday, October 23, 2008

Mpambano kupigwa Uwanja mpya
Mpambano wa Jumapili ijayo kati ya Yanga na Simba utapigwa kwenye Uwanja mkuu wa Taifa katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara inayoendelea.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Uwanja huo kuchezewa mechi hiyo ya watani wa jadi kwani Julai 27 mwaka huu mpambano wa kutafuta mshindi wa 3 wa kombe la Kagame kati ya timu hizo halikupigwa kufuatia Yanga kutopeleka timu uwanjani.

Viingilio katika pambano hilo litakaloanza saa 10 kamili jioni ni kama ifuatavyo:

VIP A: 20,000/=
VIP B: 15,000/=

VIP C: 10,000/=
Orange Straight & Curved: 5,000/=
Blue Round: 3,000/=
Green Round: 3,000/=

No comments: