Thursday, December 24, 2009

Yanga vs Simba
Ambani, Tegete na Ngassa
Hatimaye siku ya siku imefika ambapo watani wa jadi Yanga na SImba wanakutana leo katika mechi ya nusu fainali ya kombe la Tusker itakayopigwa kwanye uwanja wa Taifa Dar es Salaam

.
Pambano hilo linakuja siku 54 tu baada ya kukutana mara ya mwisho katika mchezo wa raundi ya kwanza ya ligi kuu ya Vodacom ambapo Simba ilishinda kwa 1-0. Timu zote mbili zimetamba kuibuka na ushindi katika mchezo huo.

Yanga wanajivunia rekodi yao nzuri katika michuano hya mwaka huu ya kupachika mabao tisa (9) katika mechi mbili. Mashabiki wa Simba kwa upande wao wanaipa nafasi timu yao kwa vile imepita licha ya kupangwa katika kundi gumu lililojumuisha mabingwa wa Kenya - Sofapaka na Mtibwa Sugar ya Tanzania.


Hadi sasa msahmbuiaji Jerry Tegete anaongoza kwa ufungaji kwa kupachika mabao 5 akifuatiwa na Mrisho Ngassa (2).
Mchezaji pekee ambaye yupo katika hatihati ya kucheza kwa upande wa Yanga ni Nurdin Bakari ambaye ni majeruhi.

Tusubiri dakika 90.

68 comments:

Anonymous said...

Leo tukifungwa ni bakora mtindo mmoja

Anonymous said...

CM tupe line up

Anonymous said...

leo bakora ile ile 1-0

Anonymous said...

kulikoni?

Anonymous said...

dk 23 bado 0-0

Anonymous said...

dk 23 bado 0-0

Anonymous said...

CM tupe mambo humu kuna harufu ya mnyama! ukweli mdogo hata kama tumeumia we toa,

mdau italy

Anonymous said...

tuliyeni wazee msiwe na presha...matokeo yatawekwa humu ndani

Anonymous said...

dakika 35 bado ni 0-0

Anonymous said...

halftime 0-0

Yanga imetawala 1st half lakini washambuliaji hawakuwa makini kufunga.

Ni kweli Yanga wamebadilika, wanacheza pasi nyingi

Anonymous said...

mnyama lazima aliwe huyo!

Anonymous said...

kadi za njano:
Amir Maftah na Mrisho Ngassa (YANGA)
Emmanuel Okwi na Kelvin Yondani (Simba)

Anonymous said...

LINE UP - Yanga
1. Berko
2. Nsajigwa
3. Maftah
4. Mbegu
5. Nadir
6. Bakari
7. Ngassa
8. Chuji
9. Tegete
10. Abdi
11. Kiggi

Anonymous said...

Chama la ushindi hilo jamani...halafu list ya leo imejaa watoto wa nyumbani ukiacha huyo kipa Berko,wengine wote watoto wa home!!!

Tupeni raha Yanga,ushindi wenu ndo zawadi ya Christmas kwetu mashabiki!!!

Anonymous said...

dk 60 bado 0-0

Kipa Mzungu anaingia badala ya Berko. Berko ameumizwa na Mgosi.

Anonymous said...

mbona kimya jamani...tupeni update basi mliyokuwa nyumbani...ushindi wetu tuu leo...

Anonymous said...

hapa nilipo nishapatwa na homa ya baridi tujulisheni jamaa ngapi ngapi

Anonymous said...

jamani mpira unatangazwa au la?

Anonymous said...

leo naona sarafu imesimama ngoma 0-0, mpka dk mbili zilizopita kuna mdau kanitumia text msg toka bongo

Anonymous said...

dakika ya 67 tumepata bao
Jerry Tegete

Anonymous said...

inshaallah na la pili ngasa

Anonymous said...

Yangaaaaaaaaaaaaa 1- mnyama bila, Mdau Mahenge, Wilbert, Syracuse, N.Y

Anonymous said...

msaliti Barasa anaingia badala ya Mgosi dk ya 74 bado tunaongoza 1-0

Anonymous said...

dakika 79 Simba wamerudisha kwa tuta ni 1-1 Hilary Echesa

Anonymous said...

dk 85 bado 1-1

Anonymous said...

kuna extra time au ndio matuta tena...hiyo tuta ya mnyama ilikuwa halali

Anonymous said...

cm uko wapi?

Anonymous said...

kaseja atatumaliza kwenye matuta leo

Anonymous said...

Inshaallah yanga 5 simba3 yanga fainali napaka

Anonymous said...

kilikoni tena cm lete habari kaka mpaka nione nembo yako ntaamini

Anonymous said...

dakika 90 zimekwisha 1-1

Anonymous said...

matuta sasa....
tujiandae...naona kipa mzungu ataokoa jahazi leo

Anonymous said...

sasa jamani tukilala bakora zitatembea au vipi?

Anonymous said...

bakora kamchape mkeo unasikia

Anonymous said...

sawa sawa watu wengine mahisabu yao si ya mpira kila wakiwaza bakora na wizi

Anonymous said...

sawa sawa watu wengine mahisabu yao si ya mpira kila wakiwaza bakora na wizi

CM said...

tupo kwenye extra time sasa dakika ya 92

Anonymous said...

ah!

tina said...

dakika 30 extra time imeanza...

Anonymous said...

good luck young boys

Anonymous said...

hayo matuta vipi?

CM said...

kipindi cha kwanza cha extra time kimemalizika bado ni 1-1

CM said...

dk 110 Red card Haruna Moshi

Anonymous said...

huyo mabange kwanza kajitahidi kufika bila card!

Anonymous said...

nidhamu hamna kila mechi na yanga lazima waonyeshwe card

CM said...

dakika ya 119 Shamte Ally anaipatia Yanga bao la pili.

Yanga 2 Simba 1

Anonymous said...

uzi huo huo

Anonymous said...

sherehe, hata tukosa ubingwa ushindi huu utatukomboa na kelele za hao wa-pungu

CM said...

Mnyama amelala 2-1.

Mpira umekwisha.

Yanga kucheza fainali na Sofapaka.

Ngoja tuwahi kanisani sasa

Anonymous said...

asante mola wangu.

Anonymous said...

Ahsante clinton kazi tumeona raundi ya pili ya ligi mambo yatakuwa mzuri sana washalewa bia ya crismass

Anonymous said...

YANGA HUREEEEEEEEEEEEE!
HERI YA XMAS NA MWAKA MPYA MASHABIKI WOTE WA YANGA POPOTE MLIPO DUNIANI. MLIOKO BONGO NAJUA MAJUKWAA NI YENU USIKU WA LEO!
YANGAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA

Anonymous said...

asante sana cm kwaheri mnyama! bado moja

Anonymous said...

asante sana cm kwaheri mnyama! bado moja

Anonymous said...

asante sana cm kwaheri mnyama! bado moja

Anonymous said...

bora tufungwe na nyau sio simba mzee! nani kaua yanga! nani kaua yaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaanga!
nilisema bobani kasema alibahatisha

Anonymous said...

bora tufungwe na nyau sio simba mzee! nani kaua yanga! nani kaua yaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaanga!
nilisema bobani kasema alibahatisha

Anonymous said...

Jamani Mboni Rahaaaaa!!!!!Yanga..Yanga..Yanga..Yanga..Yanga..Yanga Yanga!!!
Goli 2-1 myama yupo chalii anatapatapa....!!!
kudadadadeki sasa jama wanangu Christmas ndo imeanza!
Zawadi niliyokuwa nasuburi kutoka kwa Santa imeingia tena wakati muafaka...mboni rahaaa!!
Yanga oYee!!!

Anonymous said...

Kazi nzuri sana CM!mwenyezi akupe nguvu na maisha mema.
Jamani wanayanga itabidi tuidiskasi hiyo rahu ya Mgosi mpaka Berko akashindwa kuendelea,mii nahisi ni hujma zao simba wakizani mchawi wao ni huo kipa,kumbe mzee Papic ndio masterplan!mlioona mtupe details kama ilikuwa accidentally or intetionally tafazali!

Anonymous said...

HAPPY BIRTHDAY SIMBA SPORTS CLUB AU WANA WA MSIMBAZI


MDAU ITALY

Anonymous said...

Fisi wa kike huwa hawakosekani humu!
jama na nyie simfungue yakweni mpeane hizo besdei zenu huko??!Kha!!

Anonymous said...

Fisi wa kike huwa hawakosekani humu!
jama na nyie simfungue yakweni mpeane hizo besdei zenu huko??!Kha!!

Anonymous said...

Kesho Manji will confirm to be our next Club President....

Anonymous said...

ndugu hii coment ishajaa tupe tafsiri maana raha inazidi walitamba sana sasa naona huko nyumbani mnyama woote washalala

edwardsikawa said...

jana niliangalia mechi kuanzia dakika ya kwanza mpaka ya 124.Yanga imelamba kwa kumpata papic.Mpira wanaocheza Yanga kwa sasa hawajawai kuucheza zaidi ya miaka kumi.Yanga inacheza mpira wa kueleweka sasa hivi,hata Simba wenyewe wamekubali kwamba msimu huu Yanga ni balaa.Jana Yanga wangetulia wangewapiga Simba hata 6 bila lakini hawakuwa makini kidogo ndo maana tukapata hayo ma2.Yanga sasa hivi wana pumzi ya kucheza hata dakika 200.Jana kuanzia dakika ya 110 Simba walikuwa wanaomba mechi iishe,yaani walichoka ile mbaya.Kweli timu yetu inatia matumaini sana hata hao wakongo kwenye klabu bingwa hawatatusumbua hata kidogo.Tusubirini jpili tuwanyoe hao Sofanyau,kama mnyama tumemnyoa sharubu NYAU ndo atatushinda.KILA LA HERI YANGA.MERRY XMAS WANAYANGA WOTE.

Masebe said...

HONGERA VIJANA KWA KAZI NZURI. SALAMU ZAKE KASEJA KWANI ALISHADAI HATUWEZI KUIFUNGA SIMBA IWAPO YEYE ATAKUWA GOLINI,LABDA JANA PIA HAKUWA YEYE GOLINI. PIA HUYO MROPOKAJI BARAZA SASA AMEPATA AIBU YEYE MWENYEWE NA TIMU KIMEO ALIYOKUWA AKIISIFIA. ASANTE SANA WACHEZAJI WOTE PAMOJA NA mR.CLINTON TUMEKUKUBALI BABA.

Anonymous said...

Simba siku zote Walikuwa wanadai mechi yao na Yangaichezeshwe na mwamuzi kutoka nje juzi wamefungwa wanamlaumu mwamuzi oohh kwa nini kamwonyesha erd card Boban. Hawjui kwamba timu yao ni ya wavuta bangi kuanzia kocha na ndio maana akiingia kocha mwenye kujali nidhamu hamalizi mwezi

Anonymous said...

Wamelala wamelala hao wamelala mwamelala hao well Yanga wanagusa kama sio wao na wana Ari yaani mambo yakiwa hivi wakinusa sijui mapinduzi secon round yote wanachapwa

Yanga Imara