Saturday, January 30, 2010

Ligi Kuu ya Vodacom

Yanga vs Majimaji
Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Voodacom, Yanga leo wanajitupa katika Uwanja wa Uhuru kupambana na Majimaji ya Songea katika mchezo wa ligi hiyo.

Yanga bado wapo katika mbio za kutetea taji lake licha ya kuachwa pointi 12 na mpinzani wake mkubwa Simba ambao leo watakuwa huko Mwanza kupambana na Toto Africa ya huko.

Katika mchezo wa leo, Yanga itawakosa wachezaji wake Mrsho Ngassa (mgonjwa), Kabongo Honore(majeruhi) na Nurdin Bakari (kadi tatu za njano). Kwa hali hiyo huenda mchezaji wa kimataifa kutoka Uganda Steven Bengo akachezeshwa katika pambano la leo.

Katika mchezo wa kwanza baina ya timu hizi mbili uliopigwa huko Songea, Yanga ililala 1-0.

19 comments:

CM said...

list ya leo:
1. Obren
2. Nsajigwa
3. Maftah
4. Wisdom
5. Nadir
6. Bonny
7. Shamte
8. Chuji
9. Tegete
10. Ambani
11. Kiggi

CM said...

dk. 21 Yanga 1 Majimaji 0

Boniface Ambani

Anonymous said...

asante sana cm mwendo mdundo

italy

CM said...

HT 1-0

CM said...

mechi ya Simba na Toto Africa itachezwa kesho

Anonymous said...

nawatakia kila la kheri wana yanga wote mwendo mdundo hakijaanza kipindi cha pili kuwait ?

Anonymous said...

matokeo bado moja bila

MASEBE said...

YANGA WAMEPATA GOLI LA PILI DK YA 19 KIPINDI CHA PILI LIMEFUNGWA NA AMBANI TENA

CM said...

dk 68 Ambani amefunga mabao mawili ya haraka.

Tunaongoza 3-0. Ambani's hattrick

Anonymous said...

bado yapo magoli

Anonymous said...

naona ambani karudi ktk fomu

CM said...

dk 80 Yanga down to ten men, Wisdom Ndhlovu sent off for second bookable offence.

CM said...

dakika 90 zimemalizika kwa ushindi wa 3-0

Yanga sasa imefikisha pointi 30 ikiwa ni pointi 9 nyuma ya Simba ambayo itacheza kesho na Toto Africa.

Anonymous said...

asante saana wana jangwani asnte cm
papo kwa papo kamba hukata jiwe

italy

Anonymous said...

jamani vipi jinyama limelala kwa wanetu toto? naliombea dua mbaya lidode,

Anonymous said...

No, mnyama kashinda 3 -1, habari ndiyo hiyo, labda tungoje kwa Kagera Sugar sasa.

Anonymous said...

Hapana, mpira bado unaendelea matokeo ni kwamba Simba 0, Toto 0

CM said...

FULL TIME CCM Kirumba Mwanza Simba 2 Toto Africa 0

Mgosi dk 52, Redondo dk 54

Anonymous said...

hahaha dua yako imeota mbawa.mkubali mwaka huu hampati kitu.mnyama mkali tuu.ubingwa unatua msimbazi.oh kidedea.