Minziro kocha msaidizi Yanga
Kocha wa Ruvu Shooting, Freddy Minziro ameteuliwa kuchukua nafasi ya Salvatory Edward kuwa msaidizi wa Kostadin Papic Yanga.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga zilizopatikana Dar es Salaam jana zilisema kuwa tayari Yanga imesharidhiana na uongozi wa Ruvu Shooting, hivyo Minziro anatarajiwa kuungana na Yanga leo Zanzibar.
“Ndio hivyo, ni kweli taarifa hizo zipo kwamba Minziro sasa anakuwa msaidizi wa Papic Yanga baada ya kuonekana nafasi ya usaidizi Salva haimudu ndio maana uongozi ukaona umpe jukumu hilo Minziro,” alisema mtoa habari wetu ndani ya Yanga.
Hata hivyo huenda hiyo ndio safari ya Minziro kupewa Yanga kwani kocha Papic mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu na kuna kila dalili za kutohitajiana, si Yanga wala Papic anayemhitaji mwenzake.
Habari zilizopatikana jijini juzi zilisema kuwa kocha huyo tayari ameshaanza kufanya mchakato wa kutafuta nyingine ya kufundisha atakapoondoka Yanga na ameagiza rafiki zake sehemu mbalimbali kumfanyia kazi hiyo.
Inadaiwa kuwa kinachomfanya Papic aondoke ni hali ya kukosekana kwa morali kwa wachezaji ambao hivi karibuni waligoma wakishinikiza kulipwa sehemu ya fedha zao za usajili.
“Kocha amechoshwa, anahisi timu itafanya vibaya kwenye mashindano kwa vile wachezaji hawana morali kutokana na kudai fedha zao za usajili, pia klabu haina fedha kwa sasa kwani mfadhili wetu Yusuf Manji ni kama hayupo kwa vile hatoi tena msaada kama ilivyokuwa mwanzo na kusababisha klabu kushindwa kujiendesha”.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga zilizopatikana Dar es Salaam jana zilisema kuwa tayari Yanga imesharidhiana na uongozi wa Ruvu Shooting, hivyo Minziro anatarajiwa kuungana na Yanga leo Zanzibar.
“Ndio hivyo, ni kweli taarifa hizo zipo kwamba Minziro sasa anakuwa msaidizi wa Papic Yanga baada ya kuonekana nafasi ya usaidizi Salva haimudu ndio maana uongozi ukaona umpe jukumu hilo Minziro,” alisema mtoa habari wetu ndani ya Yanga.
Hata hivyo huenda hiyo ndio safari ya Minziro kupewa Yanga kwani kocha Papic mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu na kuna kila dalili za kutohitajiana, si Yanga wala Papic anayemhitaji mwenzake.
Habari zilizopatikana jijini juzi zilisema kuwa kocha huyo tayari ameshaanza kufanya mchakato wa kutafuta nyingine ya kufundisha atakapoondoka Yanga na ameagiza rafiki zake sehemu mbalimbali kumfanyia kazi hiyo.
Inadaiwa kuwa kinachomfanya Papic aondoke ni hali ya kukosekana kwa morali kwa wachezaji ambao hivi karibuni waligoma wakishinikiza kulipwa sehemu ya fedha zao za usajili.
“Kocha amechoshwa, anahisi timu itafanya vibaya kwenye mashindano kwa vile wachezaji hawana morali kutokana na kudai fedha zao za usajili, pia klabu haina fedha kwa sasa kwani mfadhili wetu Yusuf Manji ni kama hayupo kwa vile hatoi tena msaada kama ilivyokuwa mwanzo na kusababisha klabu kushindwa kujiendesha”.
30 comments:
pole mr minziro ,lakini karibu.
Ndio maana soka la bongo haliendelei. Yaani makocha ni walewale miaka nenda miaka rudi. Minziro ana lipi jipya? Kama ni hivyo basi mpelekeni japo Ulaya akapate mafunzo
bahili hawa watafanya nini?eti tunajilinganisha na tp mazembe,bajeti yao ya mwezi ni sawa na yanga miaka mitano ,bisha basi.
sasa imekuaje mchezo wa yanga na azam?
yang 2 azam 1..magoli yamefungwa na nsa job na idd mbaga.
yanga na ocen view wamaingia nusu
asante sana ,tafadhali unaweza kupost habari yoyote ya yanga pindi upatavyo au ya taifa stars mimi nakua na shauku kubwa kuangalia matokeo ,ntakushukuru sana .
Leo vipi nani kalal kati ya yanga na Mtibwa?
mtibwa kapigwa 2 - 1 bado mnyama. lazima achinjwe
wafungaji nani?
Jamani vipi fainali leo,mbona kimya humu.tupatie data ya mechi na mikakati jamani
Fuatilia kwenye website ya Yanga. www.yangasc.com
simba 1 sie 0, half time
Simba 2 - Yebo Yebo 0
huna adabu hata kidogo ,kwanza hakuna umeme ulipo.
Utajiju! Habari ndio hiyo. Mnyama kashapiga viwili sasa kazi kwenu.
simba 2 yeboyebo 0 gori la pili limefungwa mkina dk 62, go www.yangasc.com
DK 61: Simba wanapata goli la pili. Mfungaji Shija Mkina. Makosa ya walinzi wa Yanga.
DK 58: Kona kwa upande wa Yanga. Simba wanaokoa
DK 56: Yanga wanapata faulo. Simba wanaokoa unakuwa wa kurusha
DK 52: Godfrey Bonny anatoka anaingia Insa Job
DK 50: Isack Boakye anakosea lakini Mgosi anakuwa sio makini. Nafasi ya wazi kwa simba
Dk 48: Ochan anakosa goli, Yaw Berko anaokoa
Dk 47: Mgosi anaonyeshwa kadi ya Njano
Mpira umeanza kipindi cha pili
Visingizio vimeanza hah! hah! hah!
Si rahisi Yanga warudishe haya magoli. Wanaonekana ku-panic
Yanga ina wachezaji watatu tu waliocheza mechi ya ligi dhidi ya Simba kule Mwanza na kushinda. Simba inawakosa wachezaji watatu tu Nyoso, Kaseja na Yondani
yes hayo ndio mambo sio wewe unawaita hao yebo yebo kwani hujafundishwa adabu?
hah! hah! hah! sasa unakataa Yanga sio yeboyebo?
wewe na family yako yebo yebo.
hah! hah! hah! na bado mwaka huu yeboyebo mdebwedo. Yaani mtakata viuno kwa kwenda mbele wakati Mnyama anajinafasi!!!
nilisahau kumbe wewe punguani ,samahani kwaheri.
Mwali kapata Mume leo, Mnyama kafanya kweli. YeboYebo chaliiiii!!!!!
wape nyuma basi myama
Mpira umekwisha Yanga 0 - Simba 2..
Labda m**a yako ndio atoe!! mtalijua jiji mwaka huu!! yeboyebo mdebwedo
Yaani pamoja na million hamsini za manji Mnyama kachukua mwali!! sio mchezo!!
2 kavu bila mate leo, duuh sipati jibu maumivu ya makalio ya ma miss wa jangwani ila mmeshazoea nyinyi,another MBA lenu MWAPE ajapiga hata kishot kimoja mmeliwa tena.
neno jipla la kiswahili-YANGA-maana yake ni kutofika kwa mtu au watu kwenye sehemu au kazi kwa wakati unaotakiwa au muda uliopangiwa.
Post a Comment