Thursday, February 17, 2011

Ligi Kuu ya Vodacom

Mtihani wa Kagera Sugar leo
BAADA ya kutolewa kwenye michuano ya kimataifa mwishoni mwa wiki iliyopita, Yanga leo itakuwa kwenye Uwanja wa Kaitaba Bukoba kumenyana na Kagera Sugar ya huko katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu.

Mechi ya leo ni wakati mzuri kwa Yanga kurudisha umoja katika klabu yao ambayo imekuwa na migogoro kwa tarkiban miezi miwili sasa.

Yanga ikishinda leo itakuwa na uwezo wa kurejea kileleni mwa Ligi Kuu kwani itakuwa na pointi 35 na Simba inayoongoza sasa ina pointi 34.

Timu hizo leo zinaingia uwanjani zikiwa na historia tofauti ya mechi zake zilizopita. Kagera Sugar inaingia ikiwa inajivunia ushindi wa bao 1-0 ilioupata kwa Mtibwa Sugar, lakini Yanga inaingia uwanjani ikiwa imetoka sare ya bila kufungana na Majimaji ya Songea.

Hata hivyo, hilo linaweza lisiizuie Yanga kushinda kwani katika mechi ya mzunguko wa kwanza iliichapa Kagera mabao 2-0.

6 comments:

Anonymous said...

Bado hamna matokeo

Anonymous said...

sisi tulio nje tulie tu hamna anaetujulisha cm yupo bussy na mabomu kigamboni poleni ndugu wote wa maeneo ya karibu na tukio

CM said...

Yanga inaongoza 1-0 hivi sasa ni mapumziko

CM said...

FULLTIME: YANGA 1 KAGERA 0

Anonymous said...

kweli wachovu
N hizi ndo mvua za rasha rasha, yaani timu inataka iewe pesa na mtu asiulize pesa imetumikaje? kazi kweli kweli. Mkata kiuno hasikii mshipa kama uko ndani ha ha ha

Anonymous said...

huyo pashkuna katoka wapi?