Saturday, December 26, 2009

Fainali Tusker Challenge Cup 2009

Yanga vs Sofapaka

Fainali ya michuano ya Tusker Challenge Cup 2009 inatarajiwa kupigwa jijini Dar kwa Yanga kupambana na mabingwa wa Kenya Sofapaka.


Sofapaka - (SOte kama FAmilia kwa PAmoja Kufikia Azimio) hadi kufikia fainali imeifunga Mtibwa 3-1, imetoka sare na Simba 1-1 na kushinda mchezo wa nusu fainali dhidi ya Tusker FC 4-0.


Yanga kwa upande wake kufikia fainali imezifunga Mafunzo 6-0, Tusker FC 3-1 na kushinda mchezo wa nusu fainali dhidi ya Simba 2-1.


21 comments:

CM said...

mpira ni mapumziko hivi sasa.

Tupo nyuma kwa 1-0 lililofungwa dk ya 38 kwa freekick.

Anonymous said...

bado mapema nafasi ya kurudisha na kushinda ipo iwapo mchezo utakuwa kama walivyocheza na mnyama

Anonymous said...

ni paka hawa wakali naona tukiwadharau watatutoa nishai.wanapiga mpira

Anonymous said...

ni paka hawa wakali naona tukiwadharau watatutoa nishai.wanapiga mpira

Anonymous said...

inamaana leo hatuonani kama ck ya mnyama? tuko mbali kaka toa rada

CM said...

dk 85 tumesawazisha kupitia kwa Boniface Ambani.

Sofapaka muda wote wa 2nd half wamekuwa wakijihami.

Anonymous said...

nawatakia kila la kheri wana yanga kombe jangwani

CM said...

dakika ya 90

Tumepata bao la pili kupitia kwa Mrisho Ngassa

Tunaongoza 2-1

Anonymous said...

Big up all young africans

Anonymous said...

nilikwambieni dawa yao hao ni samaki kaka asante sana cm yamekua

CM said...

YANGA IMETWAA UBINGWA WA KOMBE LA TUSKER 2009.

YANGA 2 SOFAPAKA 1

Anonymous said...

Ahsante sana CM kwa juhudi zako pia hongera kwa ushindi huu kwa wana yanga wooooooote naomba mungu kiwango kizidi ktk raundi ya pili ubingwa jangwani inshaallah

Anonymous said...

oh! paka! limeshindwa simba jizee ndio paka?

Anonymous said...

YANGA ndio kiboko ya vijinyama vya mwituni kama paka shume ,simba alozeeka , nk. asante sana shukrani kwa wote waliowezesha. jangwani sasa bardiiiii

edwardsikawa said...

Hongereni Wanayanga wote kwa ushindi huo.Yanga sasa iko juu.

Anonymous said...

Edwardsikawa na CM na wengine wote pia nawatakia mwaka mpya mwema kwa kazi nzuri mliyokuwa mnaifanya mwaka mzima kwa kutupa taarifa muhimu za klabu yetu.Mwenyezi awape nguvu zaidi.
Yanga juu!!!
raha sana!!!
mdau USA.

pk-one said...

Yanga Daima Mbele nyuma mwiko

Anonymous said...

hongera wana yanga wote mdau cuba

Unknown said...

Kitendo cha Simba kutoleta wachezaji kuchukua medali zao ni cha kiungwana? Taratibu zinasemaje?

Anonymous said...

Taratibu gani unauliza..hakuna kitu kama hicho kwenye katiba ya kombe la tusker inayotaka timu ilete wachezaji..Mechi ingechezwa siku hiyo hiyo ya fainali then wachezaji ingebidi wabaki uwanjanai...upoo

Anonymous said...

anony wa Dec 29, 2009 12:05:00
sasa unaleta za sungura kwamba 'sizitaki mbichi hizi...' hahahaha chako ni chako tu haka kama ni mav*
mnamsusia nani? subirini mwakani muanze upya