Saturday, February 13, 2010

LIGI YA MABINGWA AFRIKA 2010

Yanga vs FC Lupopo

Safari ya wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika - Yanga inaanza leo kwa kupambana na timu ya FC Saint Eloi Lupopo ya DRC kwenye uwanja wa Taifa Dar.

Yanga inatakiwa ishinde mchezo wa leo ili kujiweka katika mazingira katika mchezo wa marudiano utakaopigwa huko Lubumbashi wiki mbili zijazo.
Mchezaji pekee ambaye ni majeruhi kwa upande wa Yanga ni winga Kabongo Honore ambaye alifanyiwa upasuaji wa goti mwanzoni mwa mwaka huu.

Kocha Kostadin Papic anatarajiwa kuteremsha kikosi chake kamili ambacho kimefanya vizuri katika mechi zake tano za mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom. Papic alifunga safari hadi Lubumbashi mwishoni mwa wiki iliyopita ili kusoma mfumo wa uchezaji wa timu hiyo ya DRC.
Kwa upande wao FC Lupopo wanadai wameisoma vizuri Yanga na walituma wawakilishi wao kuja kutazama mechi ya mwisho ya ligi dhidi ya Mtibwa Sugar ambapo Yanga iliibuka na ushindi wa 3-1.

Tusubiri dakika 90 na kama kawaida tutafahamishana kinachoendelea kutoka uwanja wa Taifa.

60 comments:

ALEX LAELA - MUGANYIZI said...

MWANA USIJISAHAU KUTUPA MATOKEO

Anonymous said...

Yanga wanapata bao la kwanza kupitia kwa Ambani katika dakika ya 5 tu. Lete raha wana wa Jangwani!!

CM said...

nipo uwanjani sasa. Mpira bado haujaanza

CM said...

Line up:
1. Berko
2. Nsajigwa
3. Maftah
4. Wisdom
5. Nadir
6. Chuji
7. Nurdin
8. Abdi
9. Ambani
10. Ngasa
11. Kiggi

CM said...

dakika ya 3 tumelambwa bao 1

CM said...

dakika ya 3 tumelambwa bao 1

Anonymous said...

yanga amefungwa tatu mpaka half time

Anonymous said...

Simba wanawashangilia sana hawa jamaa
FAN

Anonymous said...

it is still the first half and result not yet known don't get tense with what people are posting,CM will give u full updates.

MOJAONE said...

Jamani acheni kutudanganya hebu tuambieni ukweli, cc tunawategemea nyie huko kutupa habari. Kwanza kama mech itaanza saa 10 hii ina maana kuwa half time haijafika.

Anonymous said...

Mabeki wanakatika sana...
FAN

Anonymous said...

CM tu ndie wa kuaminiwa. Keep up your good work CM

MOJAONE said...

Ni kweli kabisa ndugu yangu CM ndiyo repoter wetu uwanjani na pekee ndiye tunayemwamini. shukrani sana CM kwa mchango wako huo, wewe ndio ulitakiwa upewe hii website uimantaine maana kwa ku-update tu uko NO1. Big number.

Anonymous said...

DK 21 bado 0-1.
FAN

Anonymous said...

Tumefungwa la pili dk ya 38
FAN

Anonymous said...

Mfungaji Pjilip Marufu

Anonymous said...

Simba wanawashangilia sana! Beki leo inatuangusha sana..
FAN

Anonymous said...

mpira halftime bao ni zilezile 0-2
FAN

Anonymous said...

cm vipi tunangoja ukweli kutoka kwako hawa simba wanaingia na kutupandisha presha

CM said...

halftime 0-2.

Jamaa ni wazuri mno kwenye kupanga mashambulizi.

Mtandao unasumbua sana hapa uwanjani.

CM said...

halftime 0-2.

Jamaa ni wazuri mno kwenye kupanga mashambulizi.

Mtandao unasumbua sana hapa uwanjani.

Anonymous said...

Tegete ameingia. kipindi cha pili kimeanza sasa.
FAN

Anonymous said...

msiwe na presha sisi tunaweka ukweli humu.mpira mkubali leo mpira umewashinda.mabeki wenu wote wanaharisha leo na makamasi mpaka mdomoni.naona madenga na manji wanaingia badala ya ngasa na chuji.

CM said...

ambani na Abdi wametoka huku nafasi zao zikichukuliwa na Tegete nna Bonny

Anonymous said...

Jamani kuna natumaini yoyote? Au ndio tubaki kuwa watalaam wa ligi yetu ya nyumbani? Yaani pamoja na majigambo yote ya Madega timu inaadhirika hivi? Papic anafanya nini?

Anonymous said...

Dk ya 6 Tumepata bao moja mfungaji ni Kigi Makassy. Afadhali sasa.
FAN

CM said...

kiggi Makassy anaipatia Yanga bao

Ni 1-2 dakika ya 50

Anonymous said...

Bao ni 1-2 sasa.
FAN

Anonymous said...

Tunashambulia sasa..vijana wameamka..
FAN

Anonymous said...

Dk ya 60 bado 1-2. Bengo anapasha Misuli.
FAN

Anonymous said...

Tumerudisha 2-2
FAN

Anonymous said...

sasa nyie hata kupasha misuli mnaandika mnatutia presha jamaa sisi tupo nje ya bongo hamjui tunaufatilizia vipi mpira huu

Anonymous said...

dk 24 Mrisho Ngassa anafunga bao.
FAN

Anonymous said...

Simba wako kimya sasa...
FAN

CM said...

2-2 Ngassa

Anonymous said...

wanga hao na wakae kimya wanafaida gani

Anonymous said...

DK 30 bado 2-2
FAN

CM said...

tumefungwa bao la tatu

Ndhlovumania

Anonymous said...

Tumefungwa la tatu. Bao ni 2-3 Dk ya 37. Uzembe wa mabeki tena wanajisahau sana!

Anonymous said...

Tumefungwa la tatu. Bao ni 2-3 Dk ya 37. Uzembe wa mabeki tena wanajisahau sana!

Anonymous said...

simba wanashangilia tena

Anonymous said...

Tumepigwa chuma cha nne

CM said...

kwa sisi wenye roho nyepesi tunaondoka uwanjani

Anonymous said...

Dk za majeruhi sasa.
FAN

Anonymous said...

Jamaa kwa kweli wana uwezo mkubwa.

FAN

Anonymous said...

Bao ni zile zile 2-3.
FAN

Anonymous said...

Mwanangu kazi tunayo kusonga mbele kwenye mashindano .. haya jamaa ni wazuri mnoo,
hata hao simba wengeondoka wengekua wao

Anonymous said...

Mpira umekwisha tumelala 2-3.
Mabeki tunalia nao, hawakuwa makini..

FAN

CM said...

FT 2-3

tina said...

goodbye to champion leaque maybe 2012.hahaha.mnatia aibu.labda mngecheza nao uwanja wa kaunda.

tina said...

goodbye to champion leaque maybe 2012.hahaha.mnatia aibu.labda mngecheza nao uwanja wa kaunda.

Anonymous said...

Ama kweli ng'ombe wa maskini hazai. Pamoja na full mkoko wa wageni, msaada wa maana toka kwa Manji lakini bado yeboyebo mdebwedo!! sasa mnataka msaidiwe vipi nyie?

Anonymous said...

Labda mpaka wasaidiwe na Rais JK ambae naye anaona aibu timu inavyo boa.nendeni mkajifariji na hiyo kombe ya ulevi mliyoshinda baada ya kubebwa.hakuna kitu timu imejaa uozo tupu.

Anonymous said...

simba mnafanya nini humu watani acheni wivu anzisheni blog yenu especially wale wanao-post habari za uongo hata kama mtani kama unaweka vitu vyo uongo haipendezi sio ustaarabu.

Anonymous said...

Jamaani kuna haja ya sie wenye mawazo pevu kuamka na kuibadili klabu yetu.
Kifupi jana tulicheza mpaka mwisho wa uwezo wetu ukiacha huo CM aliouita ugonjwa wa Ndlovumania.

Ok we now have a competent coach at our club, but personally I’m not happy with the way we run our team especially our future plans.

We have to bank on youth technical development, something which we don’t have at the moment.

Ukiangalia vizuri unagundua kuwa wachezaji wetu wengi hawana professional skills za kuweza kumudu soka la kisasa, na hizi wachezaji wanafundishwa kwenye academies.

SWALI la msingi,

KITU GANI KINAKWAMISHA YANGA KUTOKUWA NA ACADEMY YAKE ILIHALI JENGO LA KUKAA LIPO?

Tulisema sana wakati wa mashindano ya ligi ya U-20 ambapo katimu ketu walikuwa wanaokotana saa moja kabla ya mechi na wakaishia kufungwa kwa aibu.

Jambo jingine tuanze muda huu kuscout wachezaji wazuri wa kuwasajili mwakani ili wachukue nafasi za waliochoka.

Hili litatusaidia kuepuka usajili kama wa kina JAMA MBAA(MADEGA)

Anonymous said...

Yanga bwana hawana akili za mpira wa mashindano ya kimataifa. Wamezoea vikombe vidogo vidogo na ligi za ndani kwa msaada wa marefarii, ila wakikanyaga tu kwy anga za kimataifa ni kichapo. Kocha wenu kwa wiki nzima alikuwa akijigamba mpaka akaenda DRC kuwapeleleza, mpira hauko hivyo angalia vilabu km Man U au chelsea kila siku wanacheza na mechi zao zinaonyeshwa laivu, lkn huwezi kuwasoma na hawatabiriki na ukitiia mguu tu ni kichapo. nyinyi mumekataza eti mechi zenu za Ligi zisionyeshwe na ITV kisa wapinzani wenu watawasoma, mambo ya kizamani hayo inabidi mubadiike! Yebo yebo Mdebwedo! Kudadeki

Anonymous said...

wewe smba kalale mbele mdebwedo mama na baba yako koma kabisa kutuingilia simba tafathari kaoshe vyoo vya city

Anonymous said...

na wewe tina unatafuta bwana hakuna bwana hii ni jili ya nyanga 2 atununui mademu pole sana nenda msimbazi

Anonymous said...

mnaringa bure hakuna kitu.timu yenu mbovu.walipeni mshahara wachezaji wenu wanalia njaa wanasubiri hela ya mwezi wa januari.sijui mtafika aje DRC Congo.

Anonymous said...

Yanga haina tatizo la pesa hiyo ni furahisha kijiwe ya mapaparazi.