Asiye na mwana........
Homa ya pambano la watani wa jadi Yanga na Simba inazidi kushika kasi kufuatia tiketi za mpambano huo kuanza kuuzwa kuanzia hapo jana.
Mitaa mbalimbali ambayo nimepita leo imedhihirika kwamba hakuna shabiki ambaye anaweza kujiamini hasa ukizingatia kwamba mwenendo wa Simba si mzuri katika ligi na Yanga pia itakuwa inasumbuliwa na historia ya kutoweza kuifunga Simba kwa miaka 8 sasa.
Bila shaka yote hayo yanatoa sura ya ugumu wa pambano hilo ambalo linasubiriwa kwa hamu na wapenzi wa kandanda la Tanzania kwa muda mrefu.
Kwa wale walio Dar es Salaam ni vizuri kuwahi tiketi yako mapema ili uwe shuhuda wa mechi hiyo ya 'kufa mtu'.
Mashabiki kadhaa wa Yanga wameonekana kumpigia chapuo kipa wao Mzungu kutoka Serbia Obrev Circkovic akae golini badala ya Juma Kaseja ambaye ameidakia Simba kwa miaka 6 kabla ya kuhamia Yanga msimu huu.
Pia gumzo kubwa ni mshambuliaji Boniface Ambani ambaye amefunga mabao 13 katika mechi 9 hadi sasa. Ikiwa ni wastani wa goli 1.4 katika kila mechi.
Hata hivyo Simba licha ya mwenendo wao mbaya katika ligi mwaka huu, timu yao si ya kubeza. Kwani kwa mujibu wa Mshauri wa timu hiyo Syllersaid Mziray amesema vipaji vipo lakini tatizo lililokuwepo ni la kisaikolojia tu.
Tusubiri tuone hizo dakika 90 za mwamuzi Victor Mwandike. Mie nitakuwepo uwanjani, wewe je?
Pia gumzo kubwa ni mshambuliaji Boniface Ambani ambaye amefunga mabao 13 katika mechi 9 hadi sasa. Ikiwa ni wastani wa goli 1.4 katika kila mechi.
Hata hivyo Simba licha ya mwenendo wao mbaya katika ligi mwaka huu, timu yao si ya kubeza. Kwani kwa mujibu wa Mshauri wa timu hiyo Syllersaid Mziray amesema vipaji vipo lakini tatizo lililokuwepo ni la kisaikolojia tu.
Tusubiri tuone hizo dakika 90 za mwamuzi Victor Mwandike. Mie nitakuwepo uwanjani, wewe je?
13 comments:
Mimi niko Uingereza, sitaweza kushuhudia mechi! Nasubiri matokeo hapa.
Jamani msisahau kufunga na kuomba hawa jamaa wametutesa sana. Mungu ibariki Dar Young Africans.
Naona mzee umekung'uta VIP nimekubali. Ungechukua nyingine kama 30,000 ukawanunulie mashabiki 100.
tafadhali mwenzetu mweye blog hii, kwanza shukrani nyingi sana kutoka kwangu.pili jee itabidi ukae home ili sisi tulio mbali na tza tupate kufaidi hii match kubwa?
anony hapo juu nadhani wewe ni mgeni wa blog hii jamaa huwa anatupa matokeo "live" toka uwanjani mambo ya teke la kulia hayo wewe kesho ingia hapa utapata matokeo toka mwanzo mpaka mwisho ila naweza kupost kwenye comments..upo habari ndiyo hiyo
Katika mechi zilizopigwa leo:
Prisons 2 Azam 0
Kagera 1 Moro 0
Polisi Moro 3 JKT 3
Toto 1 Mtibwa 1
Polisi Dom 1 Villa 2
asante ,wewe unajua tena ,Nani anataka kukaa home ku miss big match.
Hawa Kagera mbona wanatutishia maisha? Jamaani mwenzenu silali jina la Mwalala linanijia usingizini.
Hata muweke shombe leo mtafungwa tu.
Manji bay bay!!!!!
Yanga 1 dk ya 15 Mwalala
Wewe bwana ambaye jina la Mwalala lililkuwa linakujia usingizini hakika kichwa ni poa. Yanga 1 dk ya 15 ni Mwalala huyo huyo. Tuombe mungu mambo yaendelee kuwa hivi hivi au tuongeze
Duh hii kali mimi ni mdau ambaye jina la mwalala lilikuwa ninanijia kichwani usiku mzima nadhani itabidi niwe mtabiri sasa.
Post a Comment